Breaking News

WANAHABARI MWANZA WAKUMBUSHWA NAFASI YAO KATIKA KUPAMBANA NA RUSHWA

Na Tonny Alphonce,Mwanza

Kulekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) mkoa wa Mwanza imeanza kutoa  elimu kwa makundi maalumu kwa lengo la kuhakikisha jamii inapinga vitendo vyote vya rushwa  na kuripoti dalili zote zinazo onyesha viashiria vya rushwa.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza James  Ruge akifungua semina ya siku moja na wanahabari wa jiji la Mwanza

Akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya siku moja kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kupambana na rushwa, Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza James  Ruge amesema vyombo vya habari vinajukumu kubwa la kuielimisha jamii juu ya rushwa na madhara yake katika ustawi wa taifa.

Baadhi ya waandishi wa habari wa jiji la Mwanza wakiwa katika semina ya siku moja ya namna gani ya kuzuia vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu

Ruge  amesema jamii inatakiwa ijue kuwa kiongozi mla rushwa akichaguliwa inamaana kuwa wananchi watakuwa wamechagua umaskini kwa kuwa kiongozi huyo hatatatua changamoto za wananchi na badala yake ataanza kujinufaisha mwenyewe.

"Kwa hiyo ndugu zangu wanahabari tumeaita leo kisheria kabisa  kwa sababu sheria ya kupambana na rushwa inaitaka TAKUKURU kushirikiana na wadau katika kutokomeza vitendo vya rushwa na ndio maana kwa umuhimu wenu tumeamua kuwaita leo tuone namna gani tutashirikiana ili kutokomeza vitendo vya rushwa.alisema Ruge"

Kwa upande wake mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Misungwi Elly Makala amesema katika kipindi hiki cha uchaguzi wananchi wanapaswa kujua  kuwa  rushwa ni kosa la jinai,ni kosa la kimaadili na pia rushwa ni kosa la kiimani hivyo katika mazingira yoyote wasikubali kupokea rushwa kutoka kwa wagombea.

Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Misungwi Elly Makala akizungumzia nafasi ya waandishi wa habari katika kupambana na rushwa.

Elly amesema Uchaguzi wa serikali za mitaa ni uchaguzi muhimu kwa kuwa viongozi wanaoenda kuchaguliwa ndio chimbuko la iutawala bora na miradi mingi inafanyika katika ngazi hiyo ya mitaa hivyo viongozi ni vema wakawa waadilifu na waliochaguliwa kihalali.

Amesema serikali za mitaa zimeanzinzwa kwa lengo la kupeleka maendeleo moja kwa moja kwa wananchi kama ibara ya 146 ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania  inavyosema.


Nae Edwin Soko mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mwanza Amewataka waandishi wa habari wasikubali kutumika katika kipindi hiki cha uchaguzi na badala yake wasimamie haki kwa wagombea wote watakaojitokeza kugombea nafasi mbalimbali.

Edwin Soko mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mwanza akiwashukuru TAKUKURU kwa kuwapatia waandishi wa habari semina ya siku moja kuhusiana masuala ya rushwa na uchaguzi

Amesema waandishi wanatakiwa kisheria  kutoa taarifa pale wanapoona vitendo vya rushwa vinafanyika na amewataka  TAKUKURU kuwalinda waandishi wanapotoa taarifa za rushwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mtaa na  uchaguzi mkuu.

Kauli mbiu ya TAKUKURU ambayo ilitolewa na mheshiwa rais inasema “Kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu,tutimize wajibu wetu” ikimtaka kila mtanzania kuwa mstari wa mbele katika kupambana na vitendo vya rushwa.

No comments