SERIKALI YAOMBWA KUINGIZA KWENYE KATIBA HAKI YA KILA MTOTO KUPEWA BIMA YA AFYA
Na Tonny Alphonce,Mwanza
Serikali
imeombwa kuingiza kwenye katiba haki ya kila mtoto anayezaliwa hapa nchini
kupewa bima ya afya kwa ustawi wa mtoto na taifa kwa ujumla.
Sophia Donald mkurugenzi wa shirika la Sauti Ya Mwanamke Ukerewe ameyaomba mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuungana kwa pamoja ili kutatua changamoto ya bima ya afya kwa watoto na walemavu.
“Kuondolewa kwa toto bima kadi kiukweli imekuwa kikwazo na ina athiri afya ya watoto kwasababu tayari tumekiuka upatikanaji wa huduma bora na rafiki kwa watoto”.alisema Sophia.
Kwa kuliona
tatizo hilo Doreen Mayani mratibu mradi kutoka Child Support Tanzania amesema
wao wanatoa huduma kwa watoto wenye ulemavu ambao wanachangamoto nyingi upande
wa matibabu kama vile kuugua kila siku,kuhitaji matibabu ya viungo ambapo wengi
wao inakuwa sio rahisi kumudu gharama za
matibabu.
Doreen Mayani mratibu mradi kutoka Child Support Tanzania akitoa mchango wake kuhusu umuhimu wa bima ya afya kwa watoto hoja iliyoibuka katika Uzinduzi wa Mradi wa Uraia Wetu unaotekelezwa na Shirika la NELICO.
Sisi kama taasisi tumesaidia watoto kupata bima ya afya mwaka jana tulitoa bima 130 kwa watoto na mwaka huu pia tumetoa bima 130 kwa watoto ambazo matokeo yake ni makubwa kwa watoto wenye ulemavu.Doreen
amesema Ili kuhakikisha watoto wanapata bima za afya wamekuwa wakiwahamasisha
wazazi na walezi kukata bima kupitia kwenye taasisi au vikundi ili waweze
kupata bima za afya kwaajili ya watoto.
Kwa upande
wake meneja Uhasiano wa shirika la New Light Children Centre Organization
(NALICO) Kwaresma Mgige amesema jambo
ambalo linaweza kufanywa na Azaki zote
ni kusimamia suala la bima ya afya kwa
mtoto liwe ni lazima kwa kila mtoto anayezaliwa kupatiwa bima ya afya.
Meneja Uhasiano wa shirika la New Light Children Centre Organization (NALICO) Kwaresma Mgige akitoa mchango wake kuhusu umuhimu wa bima ya afya kwa watoto hoja iliyoibuka katika Uzinduzi wa Mradi wa Uraia Wetu
“Tukiweza
kulichagiza hili na likaingia kwenye katiba au likatambuliwa kisheria tutakuwa tumewasaidia watoto na tukiweza
kulisimamia na likafanikiwa hili basi tutakuwa tumewaokoa watoto wote wa Tanzania hasa wale wanatoka katika familia
masikini”.alisema Qurezima.
Nae Atanasi
Evaristi kutoka Azaki ya Fadhili Teens Tanzania ameitaka serikali kuondoa
masharti iliyoweka kwa taasisi zenye nia ya kuwakatia bima watoto kwakuwa
mashariti hayo yamekuwa yakiwasababisha washindwe kuwakatia bima watoto hao licha
ya bajeti kuwepo.
Kupitia waziri
wa afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu alisema alipokuwa bungeni kuwa bima ya afya
ndio roho yahuduma za afya hapa nchini ambapo asilimia 70 ya fedha za hospitali
za serikali na binafsi zinategemea bima ya afya.
Serikali imesema baada ya kufanya uchambuzi waligundua kuwa baadhi ya vifurushi vinahatarisha uhai na uendelevu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya ikiwemo toto afya kadi ambapo matumizi yao yamekuwa makubwa kuliko michango yao hivyo kuleta hasara kwenye mfuko bima ya taifa.
“Watoto wanachangia
shilingi 54000,katika kila shilingi 100 watatumia shilingi 667 lakini la pili
kwa mwaka 2020- 2021 watoto waliosajiliwa toto afya kadi walikuwa 157920 wakachangia bilioni 5.9 na kutumia
bilioni 40.5 hii ni hasara”.alisema Ummy
Ummy
alihitimisha kwa kuagiza watoto wasajiliwe shuleni au watoto wasajiliwe pamoja
na wazazi wao ili kuwepo kwa uendelevu wa bima akitolea mfano watoto
watakaposajiliwa shuleni itakuwa rahisi
wao kwa wao kuchangiana kwenye matibabu.
No comments