Breaking News

Wazazi washauriwa kuwawekea akiba watoto wao

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Hassan Masala akizungumza na wanafunzi wa Shule mbalimbali na vyuo  katika viwanja vya furahisha  kwenye kilele cha wiki ya akiba duniani

Na Hellen Mtereko, Mwanza

Wazazi wameshauriwa kujenga utamaduni wa kuwaweka akiba watoto wao ambayo itawasaidia hapo baadae ni vema kuwashirikisha watoto na walimu ili kuweza kufahamu umuhimu wa utunzaji akiba.

Hayo yamesemwa katika  kilele cha wiki ya kuweka akiba dunia Mkoani Mwanza katika viwanja vya furahisha iliyoudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wanafunzi kutoka shule mbalimbali.

Baadhi ya viongozi walio hudhuria katika kilele hicho wamewaasa wananchi kujifunza kuweka akiba kwani imekuwawepo tabia kwa baadhi ya wananchi I kutokujali kesho yao na kuanza kuomba misaada inayotolewa kwa masimango hivyo ni vema tunaendelea kuelimisha njia sahihi ya uwekaji akiba.

Mkurugenzi Mkazi wa  Shirika lisilo la kiserikali kutoka Nchini German DSIK Tanzania Stephen Safe alipokuwa akizungumza katika mkutano huo  alisema kuwa  ilikuondokana na mitazamo hasi ni kuondokana na  misemo isiyokuwa na tija iondolewe ilikusaidia kizazi cha baadae kuwa  na muamko wa kuweka akiba.


"Tupo kwenye hatua ya mwisho tuweza kuonana na wizara husika ya Tamisemi tuingie rasmi mashuleni kwani tayali vitabu vyetu  vya elimu ya fedha vimepata baraka  zote kutoka Tanzania institute education   alisema mkurugenzi Safe.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoawa Mwanza Muhandisi Robert Gabriel Mkuu wa  Wilaya ya Ilemela Hassan Masala  alisema kuwa,ilikufikia malengo ni lazima kuweka akiba ilikufikia ndoto yako.

"Wakati huu tunaposherehekea siku ya uhamasichaji ya uwekaji akiba duniani tukumbuke kwamba huwezi kupata kitu au ndoto yako bila kuweka akiba hivyo uwe mtoto au mkubwa tujifunze kuendelea kuweka akiba ili kutimiza ndoto yako ya baadae tuache tamaa  tuwe waelevu alisema masala",

No comments