Breaking News

Wafanyabiashara wadogo watakiwa kurejea kwenye masoko

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Hassan Masala akizungumza na wafanya biashara kuhusu kurejea kwenye masoko waliyoyatelekeza kwa muda mrefu.

Na Hellen Mtereko, Mwanza

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Hassan Masala amewatoa hofu wafanyabiashara wa soko la Buzuruga kuwa  miundombinu ya soko hilo itaendelea kuboreshwa ikiwamo kutenga sehemu ya mama lishe ya kumwagia maji taka.

Masala aliyasema hayo wakati alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi ya kutembelea masoko yenye lengo la kuwataka wafanyabiashara  kurejea kwenye masoko waliyoyaacha wazi kwa muda mrefu.

Alisema kuwa lengo la Serikali ni kutaka kuona wafanyabiashara wanafanya biashara zao katika mazingira rafiki,ndio maana masoko yalijengwa ili kuweza kuepusha msongamano wa watu kulundikana barabarani.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Hassan Masala akiendelea kutoa maelekezo kwa wafanyabiashara wanaofanya biashara zao pembezoni mwa barabara


Wafanyabiashara  wakisikiliza maelekezo ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela@ Hassan Masala

" Mtakapo kuwa mmepangiwa sehemu za kwenda nendeni mkafanye biashara hatutaruhusu mtu yoyote kupanga barabarani wakati masoko yapo, Kuna athari nyingi Sana za kufanya biashara barabarani hivyo fateni maelekezo ya Serikali ili muweze kufanya shughuli zenu kwa amani",alisema masala

Aliongeza kuwa kila kitu kinakwenda kwa utaratibu sio kwamba mtakaporejea kwenye masoko hayo hamtapata wateja, watu watawafuata popote mtakapokuwa hivyo jipangeni taratibu Kama unakibanda hamisha ili usipate hasara kwa kile ulichowekeza.

Alisema , Machinga wanaofanya biashara zao ndani ya stendi wao wataendelea kufanya kwani hawazuii shughuli zingine kufanyika Wala hawazibi biashara za watu wengine hivyo wafanye kazi zao kwakufuata Sheria na taratibu zote za Nchi.

Hata hivyo kutokana na maagizo hayo ya kuwataka wafanyabiashara wote waliovamia katikati ya mji kurudi katika maeneo yao wanayostahili kufanyia biashara, Mkuu wa wilaya aliwataka Madiwani wa Halimashauri ya Ilemela kumpa ushirikiano kwani lengo ni kutaka kuona Wilaya hiyo inakuwa Safi.


No comments